Sunday 10 July 2016

Kauli za RC Paul Makonda kuhusu ugeni wa Waziri Mkuu wa India



Ni July 10, 2016 ambapo Tanzania imepata ugeni kutoka kwa Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi ambae kupitia ujio wake  ameahidi kusaidia katika utekelezaji wa Miradi ya Maji Dar es Salaam na Pwani, pia kusaidia kuendeleza sekta za Habari na Mawasiliano, Viwanda vidogo vidogo na Vya kati, Kilimo, Afya na masuala ya Usalama nchini, Ikulu  Dar es Salaam.
Baada ya Waziri hiyo kutoa ahadi hizo sasa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alisema….‘Imekuwa siku ndefu ila yenye mafanikio makubwa sana kwa Taifa langu na watanzania wote. Hongera sana Rais wetu, hongera pia Waziri Mkuu wa India’- RC Paul Makonda
Karibu tena Tanzania. Fursa zinazotafutwa na viongozi wetu naomba tuzitumie tusiishie kulalamika tu. Sasa kilimo cha mazao jamii ya kunde soko lipo tena la uhakika. kwa tani laki 1 tunaigiza dola Milioni 300, je kwa tani Milioni 7 si itakuwa dola bilioni kadhaa. Vijana tuchangamke India wanahitaji zaidi ya tani Milioni 7 ya mazao ya kunde,choroko na dengu- RC Paul Makonda

No comments: