Saturday 4 June 2016

Pumzika kwa Amani Muhammud Ali

Aliyekuwa bondia wa kwanza maarufu mweney asili ya Kiafrika, Muhammud Ali, wa Marekani amefariki leo asubuhi akiwa na umri wa miaka 74.Kulingana na msemaji wa familia yake, bingwa huyo wa zamani wa uzani wa juu, anayejulikana sana kote duniani kwa sababu ya machachari yake katika ngumi, alifariki katika jiji la Phoenix Arizona, baada ya kulazwa hospitalini Alhamisi.


Aliyekuwa bondia wa kwanza maarufu mweney asili ya Kiafrika, Muhammud Ali, wa Marekani amefariki leo asubuhi akiwa na umri wa miaka 74.Kulingana na msemaji wa familia yake, bingwa huyo wa zamani wa uzani wa juu, anayejulikana sana kote duniani kwa sababu ya machachari yake katika ngumi, alifariki katika jiji la Phoenix Arizona, baada ya kulazwa hospitalini Alhamisi.Alikuwa na matatizo ya kupumua, hali ambayo ilitatanishwa zaidi na maradhi ya Parkinson, ambayo ni hali ya mgonjwa kutetemekatetemeaka.Taarifa ya familia yake imesema kuwa ibada ya mazishi itafanywa nyumbani kwake Lousville, Kentucky.Alipozaliwa alipewa jina la Cassius Marcellus Clay.
Muhammad Ali alijiunga na masumbwi kwa bahati.


Image captionMuhammud Ali

Ali aliyekuwa na umri wa miaka 12 alikuwa na marafikize wakitafuta peremende na porp corns za bure.Na alipogundua kwamba baiskeli yake imeibwa aliagizwa kwende chini ya nyumba aliyokuwepo katika taasisi ya mafunzo ya Columbia ambapo afisa wa polisi Joe Martin alikuwa akisimamia mpango wa ndondi.Martin alimwelezea Ali kwamba angeanza kunoa ngumi zake kwa kujifunza ndondi kabla ya kumtafuta mwizi huyo.Kwa haraka alijua vile ambavyo angejichukulia na alipofika umri wa miaka 18 alikuwa ameshinda dhahabu ya Olimpiki mjini Rome.



R.I.P Ali

No comments: