Saturday 12 November 2016

Eneo Hili ndilo ambalo Mwili wa Mzee Sitta utazikwa,

Baada ya viongozi mbalimbali wa Serikali na wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam jana kuuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samuel John Sitta aliyefariki dunia November 7 2016 katika hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujerumani.

Mwili wa Samuel Sitta ulisafirishwa kwenda Dodoma ambako Wabunge, Viongozi wa Mkoa na wananchi walipata fursa ya kuuaga katika Viwanja vya Bunge na baadaye ulisafirishwa kwenda Urambo Tabora ambako maziko yanatarajiwa kufanyika leo November 12 2016 majira ya saa nane mchana.

Kwenye hii video hapa chini ni eneo ambalo Mzee Sitta atazikwa, ni eneo la kuzikwa familia ya Sitta ambalo lipo  km 2 kutoka nyumbani kwake.

No comments: