Eritrea inaadhimisha miaka 25
ya uhuru wake kutoka Ethiopia kwa sherehe kubwa mjini Asmara ambapo
miongoni mwa mengine kuna wasanii waliovalia kama wanajeshi waasi
waliopigana vita vya uhuru.
JUZI 24 MEI

Eritrea inasherehekea miaka 25 ya uhuru wake kutoka Ethiopia.

Kumekuwa pia na wasanii waliovalia kama wanajeshi waasi waliopigana vita vya miaka 30 vya uhuru

Watu wengi kutoka Eritrea huomba kupewa hifadhi katika nchi za ulaya kuliko nchi yoyote ile ya bara la Afrika.

Eritrea inakosolewa pakubwa kwa ukiukaji wa haki za binadamu.

Maelfu ya raia Eritrea wanaoishi nchi za kigeni wamerudi nyumbani kujiunga na serikali.
.

Vita kati ya Ethiopia na Eritrea pamoja na vikwazo vya kimataifa vimeiathiri nchi hiyo lakini mambo yanaonekana kuanza kubadilika.
CHANZO: BBC
No comments:
Post a Comment